Powered By Blogger

Saturday, September 7, 2013

HAYA NIDIO MAONI YA MWANAZUONI JUU YA WASANII KUPOTEZA DIRA


KWA NINI WASANII WANAOPOTEZA DIRA NA KUANGUKIA MAISHA MAGUMU WANAONGEZEKA?


HALI HALISI YA WASANII

Kutokana na matukio kadhaa yanayowapata wasanii wa mziki wa kizazi kipya, imenilazimu kufuatilia kwa makini maisha na mwenendo mzima wa wasanii. Lengo langu lilikuwa ni kutaka kujua sababu zinazowafanya wasanii kupoteza dira na kuangukia maisha magumu. Kwa haraka unaweza kujua kwamba hali hii  hutokea pale wasanii hao wanapoanguka kisanaa na kujikuta kukosa kipato kikubwa amabcho walikuwa wanakipata katika sanaa kipindi cha nyuma.

Mpaka sasa kuna wasanii kadhaa ambapo wengine wametangulia katika haki na wengine wapo katka maisha magumu yenye muambatano na mambo lukuki kama vile kujingiza katika matumizi ya madawa ya kulevya, kutumia pombe/sigara kupita kiasi na hata kujihusisha na biashara haramu. Wasanai hao wanajikuta wanaopoteza dira na kufa au kusubiri kufa huku vifo vyao vikihusishwa na mambo hayo niliyoyataja(madawa ya kulevya n.k).

SABABU ZA WASANII KUANGUKA NA KUPOTEZA DIRA

Yawezekana zikawa sababu nyingi sana za wasanii kupotea na kuanguka vibaya katika mziki lakini zifuatazo zaweza kuwa ni moja ya sababu za msingi.

1. Kuwa na uwezo mdogo wa kufikiri au kukosa elimu ya kawaida ya kuendesha maisha yao.

Wasanii wengi wanaingia katika mziki kwa kuwa wamejaliwa kipaji cha kuimba ila wengi wao hawana aidha uwezo madhubuti au elimu ya kuweza kufikiria wanafanya nini, wafanyeje, wanafanya kwa ajili gani, wanategemea nini, na wanachokifanya kinafanyweje? Hali hii hupelekea wasanii hao kufanya sanaa kwa kubahatisha na kubabaisha. Kwa hiyo mpaka mwisho wa siku anaposhuka au kuanguka kisanaa mwenyewe anashindwa kujua ni kitu kipi kimemfanya aporomoke na kitu gani afanye ili aweze kurudi kisanaa. Hali hii pia inapelekea wasanii kutosimama kidete kudai haki zao pale zinapopokonywa, kutoshirikiana na kuunda hata chama chao kitakachosimamia maslai yao kisheria. Mfano, utakuta tamasa moja, wasanii wawili wenye uwezo sawa wanalipwa kiasi tofauti. Huku ni kukosa ushirikiano na formality katika kazi yao.

2. Kuendekeza mitazamo isiyo na maana wanayoikuta katika ulimwengu wa sanaa kutoka  kwa wasanii waliotoka kabla yao.

Kuna mambo mengi ambayo sio ya msingi yanayofanywa na wasanii wengi na kuyafanya mambo hayo kama sehemu ya utamaduni wa wasanii mfano; kabla ya kupanda stejini lazima uvute bangi, msanii lazima awe na wasichana wengi, msanii kutotumia public services kama vile kupanda daladala nk., msanii kufanya shopping au kula sehemu za matawi ya juu, msanii kuvaa kwa jinsi fulani kama vile mlege(kwa wavulana) na nusu uchi (kwa wasichan). Mambo hayo yote yanapelekea wasanii wengi wanaoingia katika game kuiga pasipo kuangalia uwezo wao na madhara ya kufanya mambo hayo. Mwisho wa siku akiyumba kidogo tu katika sanaa anapata pigo moja kubwa sana kwa kuwa anakuwa hana uwezo wa kuishi kama alivyozoea. Hatimaye msanii huyo hupatwa na msongo wa mawazo na kuamua kujiingiza katika madawa ya kulevya/pombe za kupindukia eti ili kuondoa STRESS.

3.Kutowekeza katika miradi mingine yoyote

Hili ni kosa lingine kubwa linalofanywa na wasanii wengi. Mara wanapokuwa kileleni wanajisahau kwamba kuna wengine wanatamani kuwa katika killele hicho, hivyo wanajitahidi kwa hali na mali kufikia hapo walipo. Tena jitihada zinazofanywa na hao ni kubwa mno, na siku wakija kufika katika kilele hicho, wanakuwa na hasira sana kiasi kinachopelekea spidi yao kuwa kubwa sana na kumfanya yule aliye kileleni mara ya kwanza kushuka kwa spidi. Wasanii hudhani kwamba wanapokuwa juu kisanii basi wataendelea kuwa hivyo milele yote, kitu amabacho sio cha kweli. Wangekumbuka kubuni na kuwekeza katika miradi mingine ili wanaposhuka katika game wasihangaika kimaisha kwa kuwa wangepata kipato kinginge kupitia miradi yao.

Imeandikwa na:

Issaya Lupogo


Contact/Email: lupogoissaya@gmail.com

No comments: